Advertisements

Sunday, January 21, 2018

MABALOZI WATANO WAWASILISHA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO

Balozi Mteule wa Ugiriki
Balozi Mteule wa Ugiriki nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Konstantinos Moatsos (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga kabla ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho leo jijin Dar es Salaam.
Balozi Mteule wa Ugiriki nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Konstantinos Moatsos akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Ugiriki nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Konstantinos Moatsos. Mazungumzo yao yalijikita katika kuboresha ushirikiano kati ya Tanzania na Ugiriki hususan kwenye eneo la uwekezaji na biashara.



Balozi Mteule wa Mali

Balozi Mteule wa Mali nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Fafre Camara akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Mali nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Fafre Camara. Wawili hao walijadili namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiana katika kutatua changamoto za pamoja kama vile ugaidi na imani kali.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Mali nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Fafre Camara. Wengine katika picha ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afrika, Bw. Suleiman Salehe (kulia) na Afisa wa Ubalozi wa Mali.
Balozi Mteule wa Colombia
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Colombia nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Elizabeth Taylor kabla ya zoezi la kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho
.
Balozi Mteule wa Colombia nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Elizabeth Taylor akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Colombia nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Elizabeth Taylor. Wawili hao walijadili namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiana katika masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Colombia nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Elizabeth Taylor. Wengine katika picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Salvator Mbilinyi (kulia) na Afisa wa Ubalozi wa Colombia.

 Balozi Mteule wa Argentina

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Argentina nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Martin Gomez Bustillo kabla ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho.
Balozi Mteule wa Argentina nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya,  Mhe. Martin Gomez Bustillo akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Argentina nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Martin Gomez Bustillo. Wawili hao walijadili namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiana katika masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Argentina nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Martin Gomez Bustillo. Wengine katika picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Salvator Mbilinyi (kulia).
 Balozi Mteule wa Ufilipino

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mhe. Uriel Norman Garibay kabla ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho.

Balozi Mteule wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya,  Mhe. Uriel Norman Garibay akiwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga ofisini kwake jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya,  Mhe. Uriel Norman Garibay. Wawili hao walijadili namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiana katika masuala mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya,  Mhe. Uriel Norman Garibay. Wengine katika picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bibi Justa Nyange (kulia) na Afisa wa Ubalozi wa Ufilipino.

No comments: