Advertisements

Monday, January 22, 2018

ISRAEL KUSAIDIA UJENZI WA KITENGO CHA DHARURA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA


Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Dkt. Otilia Flavian Gowelle akiwa katika mazungumzo na Naibu Balozi wa Israel nchini, Mhe. Michael Baruch Baror kabla ya wawili hao hawajasaini Hati ya Makubaliano ya kushirikiana katika sekta ya Afya kati ya Tanzania na Israel. 
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bibi Dkt. Otilia Flavian Gowelle pamoja na Naibu Balozi wa Israel nchini, Mhe. Michael Baruch Baror wakiweka saini Hati ya Makubaliano ya kushirikiana katika sekta ya Afya kati ya Tanzania na Israel. Makubaliano hayo yataanza kwa kuijengea uwezo hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo Dodoma ambapo Israel itasaidia ujenzi wa Kitengo cha dharua na mifupa pamoja na ujenzi wa Kitengo cha kisasa cha wagonjwa mahututi (ICU).
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bibi Dkt. Otilia Flavian Gowelle pamoja na Naibu Balozi wa Israel nchini, Mhe. Michael Baruch Baror wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukamilisha zoezi la uwekaji saini. Watatu kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda. 

No comments: