Advertisements

Friday, January 20, 2017

MFANYABIASHARA WA MADAWA YA KULEVYA KUFIKISHWA MAHAKAMANI NEW YORK IJUMAA


Aliwasili jijini New York kwa ndege tokea Cuidad Juarez. El Chapo anakabiliwa na kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kuingiza kiwango kikubwa cha dawa za kulevya nchini Marekani.

Kiongozi huyo wa cartel ya Sinaloa alikuwa ameomba abakie Mexico lakini ombi lake limekataliwa. Yupo kwenye ulinzi mkali sababu amewahi kutoroka mara mbili kwenye magereza yenye ulinzi mkali nchini Mexico.

Atapandishwa kizimbani kwenye mahakama ya Brooklyn Ijumaa hii.

El Chapo anaaminika kujipatia mabilioni ya dola kutokana na biashara haramu ya dawa za kulevya.

source wsj.com na kwa hisani ya Mbeya Yetu

No comments: