RAIS
Jakaya Kikwete, akitoa hotuba kwenye hafla ya kuweka jiwe la msingi la
kitegauchumi PPF Plaza eneo la Vigaeni, mjini Mtwara, Oktoba 10, 2015. Jengo
hilo la ghorofa mali ya PPF litagharimu
shilingi Bilioni 9.5 ujenzi wake utakapokamilika mwishoni mwa mwaka huu.
NA
K-VIS MEDIA, MTWARA
RAIS
Jakaya Kikwete ameumwagia sifa kemkem Mfuko wa Pensehni wa PPF, kwa uwekezaji
bora, wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jingo la ghrorofatano la kitegauchumi la PPF Plaza mjini Mtwara
Oktoba 10, 2015.
“Nimefurahishwa
sana na uwekezaji wenu kwani ninaenda kustaafu na kupumzika kwa raha kutokana
na mambo makubwa mliyotafanya, nah ii ni fursa nzuri kwa uwekezaji kwenye mkoa
huu ambao utakuwa kitovu cha uchumi.” Alifafanua Rais.
Rais
Kikwete, ambaye alitua mkoani humo akitokea nchi I Msumbiji alikokwenda kuaga,
alisema, Mtwara yuko muwekezaji ambaye ni tajiri mkubwa barani Afrika
akishikilia namba moja, nay eye angependa walau kulala mkoani Mtwara wakati wa
ziara zake za kukagua miradi yake, na lakini atalala wapi, wakati hakuna hoteli
yenye hadhi yake.? Aliuliza na kuwataka wawekezaji zaidi katika eneo la
mahoteli ili kuweza kuwapokea wafanyabiashara wakubwa wanaotembelea Mtwara ivi
sasa.
Akitoa
taarifa ya ujenzi huo, Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PPF, Aggrey
Mlimuka, alisema, jingo hilo litakapokamilika ujenzi wake litagharimu kiasi cha
shilingi Bilioni 9.5 na tayari baadhi ya ghorofa zimeshachukuliwa.
Rais Jakaya Kikwete, (katikati), akipunga mkono
kuwaaga wafanyakazi wa PPF na wajenzi wa jingo la kitegauchumi la Mfuko huo “PPF
PLAZA” baada ya kuweka jiwe la msingi
Rais
Jakaya Kikwete, akimkabidhi Subira Athumani, mfano wa kadi ya uanachama kupitia
mpango wa “Wote Scheme” ambao unahusu kujiunga na uanachama kwa uchangiaji wa
hiari. (Kushoto), ni Naibu waziri wa fedha, Adam Malima, na wapili kulia ni
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, Aggrey Mlimuka
Naibu
Waziri wa Fedha, Adam Malima, akitoa hotuba kumkaribisha Rais Kikwete kuweka
jiwe la msingi la jingo la kitegauchumi la PPF mjini Mtwara Oktoba 10, 2015
Kaimu
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF, Aggrey Mlimuka,
akitoa hotuba wakati wa uwekaji jiwe la msingi la jingo la kitegauchumi la Mfuko
huo mjini Mtwara Oktoba 10, 2015
Baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake, Aggrey Mlimuka, wakiwa katika picha ya pamoja na Mwanachama mpya wa mpango wa uchagiaji wa hiari (Wote Scheme), wa Mfuko huo, Subira Athumani Makumbiri, baada ya kukabidhiwa mfano wa kadi ya uanachama
Ngoma za utamaduni nazo zilikuwepo kunogesha shughuli
Baadhi ya wafanyakazi wa PPF, na wajenzi, waimpungia mkono Rais na ujumbe wake wakati waiondoka eneo la tukio
Wajumbe wa bodi ya wadhamini ya PPF, wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Aggrey Mlimuka, (wane kulia), na wafanyakazi wa PPF, wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu, ambaye pia ni Mkurugenzi wa uwekezaji, Steven Alfred (wakwanza kushoto mstari wa mbele)
Rais
Jakaya Kikwete, (kushoto), akiangalia ushuhuda uliokuwa ukitolewa na Mwanachama
wa PPF kupitia mpango wa Wote Scheme, baada ya kuweka jiwe la msingi la
kitegauchumi la Mfuko huo mjini Mtwara Oktoba 10, 2015. Kushoto ni Makamu
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, Aggrey Mlimuka, Wakwanza kulia ni
Meneja Masoko wa PPF, Elihuruma Ngoi, na Meenja Uhusiano Lulu Mengele
Rais Kikwete, na Mama Salma Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na naibu waziri wa fedha, Adam Malima, Waziri wa Nishati, George Simbachawene, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, Wajumbe wa bodi ya wadhamini ya PPF, Wafanyakazi wa PPF, na wajenzi wa jingo la kitegauchumi la PPF Plaza mjini Mtwara leo Oktoba 10, 2015. (Picha zote na K-VIS MEDIA/Khalfan Sad)
Rais Jakaya Kikwete, (katikati), akiteta jambo
na Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya
Wadhamini, Mfuko wa Pensheni wa PPF, Aggrey Mlimuka, wakati wa hafla ya uwekaji
jiwe la msingi kwenye jingo la kitegauchumi la Mfuko huo, PPF Plaza mjini
Mtwara
Rais akisalimiana na mmoja wa wajumbe a bodi ya wadhamini ya PPF, Bi. Amelye
Rais akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PPF, ambaye pia ni Mkurugenzi wa uwekezaji, Steven Alfred
Kaimu
Mkurugezi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, ambaye pia ni Mkurugenzi wa
Uwekezaji wa Mfuko huo, Steven Alfred, akitoa hotuba wakati wa uwekaji jiwe la
msingi la jingo la kitegauchumi la Mfuko huo mjini Mtwara Oktoba 10, 2015
Jengo la kitegauchumi la ghorofa 5 linalomilikiwa na Mfuko wa Pensehni wa PPF, eneo la Vigaeni mkoani Mtwara, ambalo Rais Jakaya Kikwete, ameliwekea jiwe la msingi leo Oktoba 10, 2015
No comments:
Post a Comment