Advertisements

Tuesday, August 4, 2015

Rais Kikwete atia saini kuridhia Miswada ya Sheria mitano hadharani Ikulu, Dar es salaam

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini hati ya Muswada wa Sheria ya Mafuta na Gesiasilia Jumanne, Agosti 4, 2015 katika Ukumbi mpya wa Ikulu, Dar Es Salaam akishuhudiwa na Waziri wa Nishati na Madini Mhe George Simbachawene na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Ngosi Mwihava
Rais Kikwete akipeana mikono na Waziri wa Nishati na Madini Mhe George Simbachawene baada ya kuweka saini kuridhia Muswada wa Sheria ya Mafuta na Gesiasilia Jumanne, Agosti 4, 2015 katika Ukumbi mpya wa Ikulu, Dar Es Salaam
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kuridhia Muswada wa Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesiasilia Jumanne, Agosti 4, 2015 katika Ukumbi mpya wa Ikulu, Dar Es Salaam akishuhudiwa na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya na Katibu Mkuu wizara hiyo Dkt. Servacius Likwelile
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya baada ya kuweka saini kuridhia Muswada wa Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesiasilia Jumanne, Agosti 4, 2015 katika Ukumbi mpya wa Ikulu, Dar Es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Katibu Mkuu Waziri wa Fedha Dkt. Servacius Likwelile baada ya kuweka saini kuridhia Muswada wa Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesiasilia Jumanne, Agosti 4, 2015 katika Ukumbi mpya wa Ikulu, Dar Es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kuridhia Muswada wa Tume ya Walimu Jumanne, Agosti 4, 2015 katika Ukumbi mpya wa Ikulu, Dar Es Salaam akishuhudiwa na Dkt. Shukuru Kawambwa ambaye ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Sifuni Mchome
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa baada ya kuweka saini kuridhia Muswada wa Tume ya Walimu Jumanne, Agosti 4, 2015 katika Ukumbi mpya wa Ikulu, Dar Es Salaam kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Sifuni Mchome

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome baada ya kuweka saini kuridhia Muswada wa Tume ya Walimu Jumanne, Agosti 4, 2015 katika Ukumbi mpya wa Ikulu, Dar Es Salaam

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katika picha ya pamoja na Mheshimiwa George Simbachawene, Waziri wa Nishati na Madini, Mheshimiwa Saada Mkuya, Waziri wa Fedha na Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi baada ya hafla ya kuweka saini na kuridhia miswada ya Sheria ya Mafuta na Gesiasilia, Muswada wa Uwazi na Uwajibikaji, Muswada wa Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesiasilia, Muswada wa Masoko ya Bidhaa na Muswada wa Tume ya Walimu.

PICHA NA IKULU

No comments: