Advertisements

Thursday, August 27, 2015

MISS TANZANIA YAPATA MWENYEKITI MPYA

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundega akiongea na wanahabari (hawapo pichani).

Kamati inayosimamia mashindano ya Miss Tanzania Lino International Agency imepata Mwenyekiti na wajumbe wapya watakaoandaa, kuratibu na kusimamia mashindano ya urembo ya Miss Tanzania.
Akiwatambulisha wajumbe hao mbele ya waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam, aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania iliyomaliza muda wake Hashim Lundenga amesema kuwa kamati mpya ndiyo itakayowajibika na shughuli zote zilizokuwa zikifanywa na kamati ya awali.

Amesema kamati hiyo itafanya kazi zake kwa kuzingatia sheria na vigezo vyote vya kimaadili ili kuepuka ukiukwaji wa taratibu za mashindano hayo.

“Hatutamvumilia mwanakamati yeyote atakayevunja miiko ya mashindano haya, sisi tutakuwa nyuma tukiangalia kwa umakini”, amesema Bw. Lundenga.

Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa kamati hiyo Juma Pinto ametoa pongezi za dhati kwa kamati iliyomaliza muda wake na kuhaidi kukubaliana na mfumo unatumika kuratibu mashindano hayo .
“Namshukuru Lundenga kwa kunikabidhi nafasi hii ya mwenyekiti wa kamati ya miss Tanzania, naahidi kuratibu mashindano haya kwa kuzingatia vigezo na masharti yaliyowekwa ili kamati yangu iweze kukidhi haja ya mashindano haya”. Amesema.

Naye Msemaji Mkuu wa kamati hiyo na aliyekuwa Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006 Jokate Mwegelo, ametoa rai kwa wasichana wa kitanzania wajitokeze kushiriki mashindano hayo kwa kuonesha vipaji walivyonavyo na kupata ajira.

Mwishoni mwa mwaka jana Mashindano ya Miss Tanzania yalikumbwa na mtafaruku wa ukiukwaji wa maadili na vigezo vya mashindano na kulazimika kusimamishwa kwa muda na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA).

Kamati Mpya ya Miss Tanzania inaundwa na wajumbe wafuatao

1.Juma Pinto – Mwenyekiti

2.Lucas Rutta – Makamu Mwenyekiti

3.Doris Mollel – Katibu Mkuu

4.Jokate Mwegelo – Msemaji wa Kamati

5.Hoyce Temu – Mjumbe

6.Mohamed Bawazir – Mjumbe

7.Gladyz Shao – Mjumbe

8.Magdalena Munisi 0 Mjumbe

9.Shah Ramadhani – Mjumbe

10.Hamm Hashim – Mjumbe

11Khalfani Saleh – Mjumbe

12.Ojambi Masaburi – Mjumbe

Kwa upande wa Sekretariet tunao wajumbe 4 ambao ni

1.Dr.Ramesh Shah

2.Hidan Ricco

3.Yasson Mashaka

4.Deo Kapteni

-mwisho-

No comments: