Advertisements

Thursday, July 2, 2015

DEGE ECO - VILLAGE WASHIRIKI MAONYESHO YA SABASABA, WAWAOMBA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KUNUNUA NYUMBA

Mradi wa nyumba unaosimamiwa na kampuni ya Hifadhi inayoitwa Dege Eco-Village umeshiriki Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa Jijini Dar es Salaam ya Saba Saba.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,  Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo Bw. Azhar Malik wa Dege eco-Village alisema “Kwa sasa ujenzi unaendelea na karibu aina ya nyumba apartment 3000 zishakamilika.
Aliongezea kusema kwamba kupitia mradi huu waTanzania watanufaika kwa kupata ajira na pia kuwa na huduma kama hospitali, shule, maduka eneo la Kigamboni.
Mradi huu unajengwa kwenye eneo takriban eka 300 na kampuni hiyo imewekeza zaidi ya dola milioni 350. Kwa ujumla nyumba aina ya villa ziko 300 na apartment ziko 7400. Mradi huu utakamilika mwaka 2018. Apartment zitakamilika mwaka 2017 na villa mwaka 2018.
Ndani ya mji huu wa Dege Eco-Village wa kazi hawatahitaji kwenda popote kwasababu kila kitu kitakuwepo kama shule za watoto, kituo cha polisi, hospitali, supermarket, na kadhalika.
 
Wafanyakazi wa Dege Eco - Village akimhudumia wateja wao aliyefika katika banda lao.
Wafanyakazi wa Dege Eco - Village wakiwahudumia wateja wao waliofika katika banda lao.
Muonekano wa Banda lao lililopo viw
 
Wafanyakazi wa Dege Eco - Village akimhudumia wateja wao waliofika katika banda lao.
Wafanyakazi wa Dege Eco - Village amkimpa maelekezo mteja aliyefika bandani kwao kuchangamkia fursa ya kununua nyumba.
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo Bw. Azhar Malik wa Dege Eco-Village (katikati) akiwaonyesha wafanyakazi wa kampuni hiyo namna walivyoweza kufanya vyema katika mauzo ya nyumba.
Wafanyakazi wakiwa katika picha ya pamoja.

No comments: