Advertisements

Friday, October 24, 2014

MAMA TUNU PINDA MGENI RASMI KATIKA MKUTANO WA AKINA MAMA WA KITANZANIA WAISHIO UINGEREZA

Mgeni rasmi Mama Tunu Pinda akisalimiana na Mwenyekiti wa TAWA UK Bi Mariam Kilumanga , alipowasili katika Balozi zaTanzania Uingereza. Nyuma ya Mama Tunu ni Mwenyeji wake Mama Joyce Kallaghe na pembeni Afisa Mkuu Kiongozi wa Ubalozi Caroline Chipeta.
Mama Tunu Pinda akiweka sahihi kwenye kitabu cha wageni Ubalozini , huku mama Kalaghe akiangalia.
Mama Tunu kati akiwa na Mwenyeji wake kushoto Mama Joyce Kallaghe na kulia Mtoa Mada ya fursa na Uwekezaji aliyeambatana na mama Tunu Tanzania Women Chamber of Commerce Mama Anna Matinde.
Baadhi ay Wanawake waliohudhuria wakimkaribisha Mama Tunu na Mama Matinde.
Katibu wa Tanzania Women Association Uk (TAWA UK ) Bi Mariam Mungula akiongea machache kuwakaribisha wageni.
Mama Joyce Kallaghe , ambaye pia ni Mlezi wa TAWA UK , akifungua Mkutano rasmi na kuwatambulisha wageni wake.
Mama Anna Matinde akiongea na akina mama mambp mengi ya kusisimua na kuhamasisha aliyokuwa nayo kuhusu Uwekezaji nyumbani Tanzania.
Baadhi ya akina mama wenye shauku kubwa wakimsikiliza mama Matinde kwa makini.
Mama Tunu Pinda aliposimama kuongea na akina mama na kufunga Mkutano.
baadhi ya Wakina mama washiriki wakipata picha na wageni rasmi.
Maafisa wa Ubalozi wanawake katika Picha ya upendeleo na wageni wao.
Wageni na Uongozi wa TAWA UK walioandaa Mkutano huo.

Mama Tunu Pinda alikuwa Mgeni rasmi katika Mkutano cha akina mama wa Kitanzania waishio Uingereza , Kilichoandaliwa na Kikundi cha Umoja wa Wanawake kiitwacho Tanzania Women Association UK (TAWA UK).

Mama Tunu Pinda alihudhuria Mkutano huo kwa mualiko wa mwenyeji wake Mrs Joyce Kallaghe Mke wa Balozi wa Tanzania Uk, Peter Kallaghe.

Mtoa mada aliyeongozana na Mama Tunu , alikuwa ni Mama Anna Matinde , mwanamke Mjasiriamali mahiri na aliyebobea ambaye ana kofia mbalimbali za Uwakilishi wa Wanamke na kibiashara katika taasisi tofauti za sekta Binafsi ikiwemo na kuwa Mkurugenzi wa Tanzania Women Chamber of Commerce.

Mama Matinde licha ya kuwatia moyo akina mama na kuwahamasisha wajikite kwenye biashara Binafsi na kubadilishana Ujuzi kutoka Tanzania na Uingereza, vilevile aliwapa somo la Uwekezaji na pamoja na kuainisha Fursa nyingi za kuwekeza zilizopo nyumbani Tanzania. Baada ya kikao wanawake wengi walioyeshwa kuridhika na ushauri wa mama Matinde.

Mgeni rasmi Mama Tunu Pinda aliwahimiza akina mama vilevile wasisahau kuwekeza nyumbani hat kama wako nje ya Nchi, na kuwahakikishia kwamba sasa hivi mwanamke wa Kitanzania anaelekea kuwa na haki sawa za umiliki ardhi na mali kama ilivyoainishwa katika Katiba Iliyopendekezwa endapo itapita kwa wananchi, Hivyo aliwasihi akina mama hao wasiwe na woga wa kuwa na mali kutokana na baadhi ya mila kwani Katiba itawalinda.

Mkutano huu uliofana ulimalizika kwa ahadi ya Uongozi wa TAWA UK walioratibu Kikao hiki kuwa watafanya Mkutano Mkubwa Zaidi wa Uwekezaji na Fursa kwa Akina Mama Muda si mrefu.

No comments: