Advertisements

Friday, July 25, 2014

RAIS KIKWETE AMUAPISHA JAJI KIONGOZI WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete akimuapisha Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila leo jijini Dar es Salaam.
Jaji kiongozi wa mahakama kuu ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Jaji Shaban Ally Lila akitia saini hati ya kiapo mbele ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa hafla ya kuapishwa kwake leo Dar es Salaam, kati mwenye miwani ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akishuhudia tukio hilo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Jakaya Kikwete akiweka saini hati ya kiapo ya Jaji Mkuu wa mahakama kuu ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Jaji Shaban Ally Lila wakati hafla ya kuapishwa kwake jaji huyo jiji Dar es Salaam leo.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Jakaya Kikwete akimkabidhi hati ya kiapo Jaji mkuu wa mahakama kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jaji Shaban Ally Lila wakati wa hafla ya kuapishwa kwake jaji huyo jijini Dar es Salaam leo.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akimpongeza Jaji Kiongozi wa mahakama kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jaji Shaban Ally Lila mara baada ya kuapishwa kwake katika hafla iliyofanyika Ikulu leo.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania Mhe. Shaban Ally Lila akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Majaji wa Mahaka Kuu Tanzania mara baada ya kuapishwa rasmi kushika wadhifa huo katika hafla iliyofanyika Ikulu leo jijini Dar es Salaam.Kushoto kwake ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman.Picha zote na Frank Shija- MAELEZO

No comments: