Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania Dkt
Agnes Kijazi akikabidhi baadhi ya vifaa vilivyotolewa na Chama cha Watanzania
Waishio Geneva-USWISI (TAS).
Watoto wa kituo cha
Amani Orphanage Centre wakifurahia baadhi ya vifaa vilivyotolewa na TAS
Aidha Dkt Kijazi alisema
TAS wameendelea kuonyesha moyo wa upendo
kwani hivi karibuni wametoa msaada wa fedha (Tshs 500,000) kwa Mama Aida wa
Mbeya aliyejifungua wototo wanne mwanzoni mwa mwaka huu. Msaada huo
uliwasilishwa kwa niaba ya TAS na meneja wa TMA kanda ya nyanda za juu kusini
magharibi Bwana Issa Hamad.
Akipokea msaada huo
msimamizi na mwanzilishi wa kituo cha Amani Bi. Margareth Mwegalawa aliwashukuru watanzania wote waishio Geneva
kwa kuwakumbuka watoto wa Amani hata kuwawezesha kupata baadhi ya mahitaji
waliokuwa wanahitaji, na alimuomba Dkt Kijazi kuwasilisha salamu hizo kwa
kusisitiza msaada huo sio mdogo bali ni mkubwa sana kulingana na uhitaji wake. Bi.
Magreth alisema kituo chicho kina watoto 37 wakiwa wasichana 25 na wavulana 12
wenye umri kati ya mwaka mmoja (1) na miaka kumi na tano (15).
Akizungumza kwa niaba
ya watoto wa Amani Orphanage Centre mtoto Beatrice Phine alisema sote
tunafurahi kwa kupata tank la maji, viti na meza ambavyo vitaboresha maisha
yetu na mazingira ya kusomea. Alimuomba Dr. Kijazi awafikishie salaam zao za
upendo na shukrani kwa TAS.
No comments:
Post a Comment