KATIKA kuelekea sikuu za Krismasi na Mwaka mpya pilika pilika
zimeongezeka katika mji wa Moshi na mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla huku
vibaka pia wakiendelea na udokozi na wizi wa vitu mbalimbali.
Katika kuthibitisha hilo juzi Tanzania Daima limeshuhudia mkazi wa
kijiji cha Nshara, Machame wilayani Hai,ambaye jina lake halikupatikana
mara moja amenusurika kuuawa kufuatia kipigo kutoka kwa wananchi wenye
hasira kumshambulia kwa silaha za jadi baada ya kuiba kitoto cha nguruwe
maarufu kama "Kiti moto".
Tukio hilo la aina yake ambalo linaashiria maandalizi ya siku kuu hizo
lilitokea juzi majira saa 5.30 asubuhi kijijini humo baada ya mkazi huyo
kuonekana akiwa amembeba mnyamya huyo begani akiwa katika mfuko,maarufu
kama Sandarusi mithili ya mzigo wa kawaida.
Akizungumzia tukio hilo,mkazi wa kijiji cha Nshara, Husein Mbaruku
alisema mtu huyo alionekana akinyata katika banda la Nguruwe akiwa na
mfuko wake akiamini kuwa hakuna mtu aliyemuona ingawa wenyeji nao
walikuwa wakimvizia ili kuona anachotaka kufanya.
KATIKA kuelekea sikuu za Krismasi na Mwaka mpya pilika pilika
zimeongezeka katika mji wa Moshi na mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla huku
vibaka pia wakiendelea na udokozi na wizi wa vitu mbalimbali.
Katika kuthibitisha hilo juzi Tanzania Daima limeshuhudia mkazi wa
kijiji cha Nshara, Machame wilayani Hai,ambaye jina lake halikupatikana
mara moja amenusurika kuuawa kufuatia kipigo kutoka kwa wananchi wenye
hasira kumshambulia kwa silaha za jadi baada ya kuiba kitoto cha nguruwe
maarufu kama "Kiti moto".
Tukio hilo la aina yake ambalo linaashiria maandalizi ya siku kuu hizo
lilitokea juzi majira saa 5.30 asubuhi kijijini humo baada ya mkazi huyo
kuonekana akiwa amembeba mnyamya huyo begani akiwa katika mfuko,maarufu
kama Sandarusi mithili ya mzigo wa kawaida.
Akizungumzia tukio hilo,mkazi wa kijiji cha Nshara, Husein Mbaruku
alisema mtu huyo alionekana akinyata katika banda la Nguruwe akiwa na
mfuko wake akiamini kuwa hakuna mtu aliyemuona ingawa wenyeji nao
walikuwa wakimvizia ili kuona anachotaka kufanya.
No comments:
Post a Comment